Ajira

Nafasi 8 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

Nafasi 8 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

Nafasi 8 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa 2025

Nafasi 8 za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa: Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa ametangaza nafasi mpya 8 za ajira baada ya kupokea kibali kutoka kwa Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – Utumishi. Watanzania wote wenye sifa wanakaribishwa kuomba nafasi hizi kwa kuzingatia vigezo vilivyoainishwa hapa chini.

Nafasi za Kazi Zilizotangazwa

1. Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja la II – Nafasi 5

Majukumu:

  • Kuchapa barua na nyaraka mbalimbali, zikiwemo za siri
  • Kupokea wageni na kuelekeza wapi watapokea huduma
  • Kutunza kumbukumbu za matukio, ratiba, na miadi ya ofisi
  • Kupanga na kuandaa vikao
  • Kuandaa orodha ya vifaa vya ofisi
  • Kusambaza majalada na taarifa muhimu kwa idara husika

Sifa za Mwombaji:
Awe na elimu ya kidato cha nne pamoja na stashahada (Diploma) au cheti cha NTA Level 6 katika Uhazili. Lazima awe amefaulu Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza (100 maneno kwa dakika), na awe na ujuzi wa matumizi ya programu za ofisi kama Word, Excel, PowerPoint, E-mail, na Publisher kutoka chuo kinachotambuliwa na serikali.

Mshahara: Ngazi ya TGS C

2. Dereva Daraja la II – Nafasi 3

Majukumu:

  • Kukagua magari kabla na baada ya safari
  • Kuwapeleka watumishi katika safari za kikazi
  • Kufanya matengenezo madogo ya magari
  • Kusambaza nyaraka na kutunza logbook
  • Kusafisha gari na kutekeleza majukumu mengine ya udereva

Sifa za Mwombaji:
Awe na elimu ya kidato cha nne pamoja na leseni ya daraja E au C aliyotumia kwa zaidi ya mwaka mmoja bila ajali. Lazima awe na vyeti vya mafunzo ya udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na serikali.

Mshahara: Ngazi ya TGS B1

Vigezo vya Jumla kwa Waombaji

  • Awe raia wa Tanzania mwenye umri kati ya miaka 18 hadi 45
  • Ambatishe cheti cha kuzaliwa na wasilisha CV iliyo na namba za simu na majina ya wadhamini
  • Ambatishe vyeti vya kitaaluma na vya kidato cha nne au sita kulingana na kazi unayoomba
  • Leseni ya daraja E au C lazima iambatishwe na cheti cha mafunzo ya udereva
  • Testmonials na Statement of Results hazitakubalika
  • Weka picha ya β€œpassport size” kwenye mfumo wa Ajira
  • Waombaji waliomaliza masomo nje ya nchi wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na TCU, NECTA, au NACTE
  • Wastaafu hawaruhusiwi kuomba bila kibali rasmi
  • Walioko kwenye nafasi za kuingilia katika Utumishi wa Umma hawapaswi kuomba
  • Atakayetoa taarifa za uongo atachukuliwa hatua za kisheria

Tarehe ya Mwisho ya Kutuma Maombi

Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 13 Julai 2025.

πŸ”” Je? unatafuta Nafasi za Kazi? Jiunge na Watanzania wengine kupitia WHATSAPP CHANNEL kwa matangazo ya ajira kila siku!

🌐 Tembelea Habari Wise kwa habari mpya kila siku!