MUHAS Yatoa Orodha ya Walioitwa Kazini Agosti 2025
Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kimetoa taarifa rasmi kwa waombaji kazi waliopitia usaili mnamo tarehe 19 hadi 20 Mei, 2025. Kupitia tangazo hilo, MUHAS imetaja majina ya waliofaulu usaili na kuitwa kuanza mchakato wa ajira rasmi.
Ajira Kufanyika Baada ya Uhakiki wa Vyeti
MUHAS imeeleza kuwa ajira kwa waliofaulu zitathibitishwa endapo tu vyeti vyao vitahakikiwa na mamlaka husika. Hii ni hatua ya kuhakikisha kuwa nyaraka zote zinazowasilishwa ni halali na sahihi kabla ya kupewa barua ya ajira.
Walioitwa Wajitokeze Tarehe 6–7 Agosti 2025
Waombaji waliotajwa wanapaswa kufika chuoni tarehe 6 na 7 Agosti 2025 kuanzia saa 3:00 asubuhi kwa ajili ya kukamilisha taratibu za ajira. Watatakiwa kufika na nyaraka muhimu zilizoorodheshwa kwa ajili ya uhakiki.
Nyaraka Muhimu za Kuwasilisha
Waombaji wote walioitwa wanapaswa kuwa na:
(i) Vyeti Halisi na Nakala Zilizothibitishwa
Vyeti vya kitaaluma kuanzia kidato cha nne pamoja na nakala mbili zilizothibitishwa na wakili au hakimu.
(ii) Cheti cha Kuzaliwa
Kitahitajika kwa ajili ya kuthibitisha taarifa za msingi za mhusika.
(iii) Nakala ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA)
Ni muhimu kwa utambuzi rasmi wa kijamii na kisheria.
(iv) Picha Ndogo Tatu za Rangi
Passport size (3) zitakazotumika katika kumbukumbu za kiutumishi.
Kwa Waliokosa Nafasi
MUHAS imewasihi wale ambao majina yao hayakutajwa katika orodha hii kutokata tamaa bali kuendelea kuomba nafasi pindi zitakapotangazwa tena.
Pakua Orodha Kamili ya Majina ya Walioitwa Kazini MUHAS hapa:
BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD PDF YA TANGAZO
🔔 Tafuta Nafasi za Kazi? Jiunge na Watanzania wengine kupitia WHATSAPP CHANNEL kwa matangazo ya ajira kila siku!
🌐 Tembelea Habari Wise kwa habari mpya za ajira kila siku!