Elimu

Kozi za VETA 2025, Orodha Kamili Na Gharama zake

Kozi za VETA 2025, Orodha Kamili Na Gharama zake

Orodha ya Kozi za VETA na Gharama Zake 2025

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) inaendelea kuimarisha maendeleo ya ujuzi nchini kwa kutoa kozi mbalimbali zenye mwelekeo wa vitendo. Kozi hizi zimegawanyika katika makundi mawili: muda mrefu na muda mfupi, na zinalenga kuongeza fursa za ajira kwa vijana wa Kitanzania.

Kozi za Muda Mrefu VETA 2025

Kozi hizi huchukua kati ya miezi 3 hadi 6, kulingana na fani unayochagua. Ada ya mwanafunzi wa kutwa ni TSh 60,000 na kwa mwanafunzi wa bweni ni TSh 120,000. Gharama nyingine zinazohusiana na vifaa na huduma hulipwa kati ya TSh 200,000 hadi 250,000 kutegemeana na chuo na kozi husika.

Mifano ya Kozi za Veta za Muda Mrefu

Ufundi wa Magari

  • Muda: Miezi 6
  • Ada: TSh 355,000
  • Chuo: VETA Chato

Umeme wa Majumbani

  • Muda: Miezi 6
  • Ada: TSh 355,000
  • Chuo: VETA Chato

Ushonaji wa Nguo

  • Muda: Miezi 5
  • Ada: TSh 355,000
  • Chuo: VETA Chato

Matumizi ya Kompyuta

  • Muda: Miezi 3
  • Ada: TSh 165,000
  • Chuo: VETA Chato

Ufundi Bomba

  • Muda: Miezi 6
  • Ada: TSh 355,000
  • Chuo: VETA Chato

Kozi za VETA za Muda Mfupi 2025

Hizi ni kozi zinazochukua wiki 1 hadi miezi 3, zikitolewa kwa ajili ya kuwapa wahusika ujuzi wa haraka katika fani maalum. Ada za kozi hizi zinatofautiana kati ya TSh 50,000 hadi 320,000 kutegemeana na kozi na chuo.

Mifano ya Kozi za Muda Mfupi

Udereva wa Awali

  • Muda: Wiki 5
  • Ada: TSh 200,000
  • Chuo: VETA Mbeya

Udereva wa Magari ya Abiria (PSV)

  • Muda: Wiki 2
  • Ada: TSh 200,000
  • Chuo: VETA Mbeya

Udereva wa Pikipiki na Bajaji

  • Muda: Wiki 2
  • Ada: TSh 70,000
  • Chuo: VETA Mbeya

Uhazili (Kompyuta na Sekretarieti)

  • Muda: Miezi 3
  • Ada: TSh 200,000
  • Chuo: VETA Mbeya

Tecknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT)

  • Muda: Miezi 5
  • Ada: TSh 600,000
  • Chuo: VETA Mbeya
Orodha ya Kozi za VETA na Gharama Zake 2025
Orodha ya Kozi za VETA na Gharama Zake 2025

Utaratibu wa Kujiunga na Kozi za VETA

Kwa yeyote anayetaka kujiunga na mafunzo ya VETA, ni muhimu kufuata taratibu rasmi zifuatazo:

Hatua za Kujiunga

1. Kupata Fomu ya Maombi

Fomu zinapatikana kwenye vyuo vya VETA au kupitia tovuti yao rasmi.

2. Kujaza Fomu kwa Usahihi

Hakikisha taarifa zako zote zimejazwa kikamilifu na kwa usahihi.

3. Kuambatisha Nyaraka

Ambatanisha nakala ya cheti cha elimu, cheti cha kuzaliwa, na picha za pasipoti.

4. Kuwasilisha Maombi

Wasilisha fomu kamili pamoja na nyaraka zote kwenye chuo husika cha VETA unachotaka kujiunga nacho.

5. Kufanya Mtihani wa Kujiunga

Baada ya kuwasilisha maombi, utahitajika kufanya mtihani wa kujiunga kama sehemu ya mchakato wa kuchagua wanafunzi.

VETA inaendelea kuwa chaguo bora kwa watanzania wanaotaka kupata elimu ya ufundi yenye tija na inayolingana na soko la ajira.

🔔 Je? unatafuta Nafasi za Kazi? Jiunge na Watanzania wengine kupitia WHATSAPP CHANNEL kwa matangazo ya ajira kila siku!

🌐 Tembelea Habari Wise kwa habari mpya kila siku!