TFF Yatangaza Uchaguzi Mkuu 2025
Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imetangaza rasmi kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa TFF mnamo tarehe 16 Agosti 2025, ambapo zoezi hilo litaandaliwa jijini Tanga.
Nafasi Zinazogombewa
Katika uchaguzi huu muhimu, nafasi zifuatazo zitakuwa wazi kwa wagombea:
- Rais wa TFF – Nafasi 1
- Wajumbe wa Kamati ya Utendaji – Nafasi 6
Gharama za Kuchukua Fomu
Kwa wote wanaotaka kugombea, gharama za kuchukua fomu ni kama ifuatavyo:
- Rais – Shilingi 500,000
- Wajumbe wa Kamati ya Utendaji – Shilingi 200,000
Tarehe ya Kuchukua Fomu
Fomu za kugombea zitapatikana kuanzia Jumatatu, tarehe 16 Juni 2025 hadi Ijumaa, tarehe 20 Juni 2025. Mwisho wa kuchukua fomu ni saa 10:00 jioni.
Mahali Fomu Zinapopatikana
Fomu zinapatikana kupitia njia zifuatazo:
- Makao Makuu ya TFF
- Website ya TFF (www.tff.or.tz)
Maelekezo ya Malipo
Malipo yote ya fomu yanapaswa kufanyika kupitia Benki ya NBC kwa kutumia maelezo yafuatayo:
- Akaunti Namba: 012103025707
- Jina la Akaunti: Tanzania Football Federation
MUHIMU: Wakati wa kurejesha fomu yako ya kugombea, ambatanisha risiti ya malipo (Pay-in slip) kama uthibitisho wa ulipaji.
Ikiwa unakusudia kushiriki katika kuongoza mustakabali wa soka nchini, huu ndio wakati wako. TFF inatoa wito kwa watu wenye sifa stahiki kujitokeza na kushiriki mchakato huu wa kidemokrasia.

